Proverbs 9:1-6
Makaribisho Ya Hekima Na Ya Upumbavu
1 aHekima amejenga nyumba yake;
amechonga nguzo zake saba.
2 bAmeandaa nyama na kuchanganya divai yake;
pia ameandaa meza yake.
3 cAmewatuma watumishi wake wa kike, naye huita
kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 dAnawaambia wale wasio na akili,
“Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 eNjooni, mle chakula changu
na mnywe divai niliyoichanganya.
6 fAcheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi;
tembeeni katika njia ya ufahamu.
Copyright information for
SwhKC