Proverbs 9:1-6

Makaribisho Ya Hekima Na Ya Upumbavu


1 aHekima amejenga nyumba yake;
amechonga nguzo zake saba.

2 bAmeandaa nyama na kuchanganya divai yake;
pia ameandaa meza yake.

3 cAmewatuma watumishi wake wa kike, naye huita
kutoka mahali pa juu sana pa mji.

4 dAnawaambia wale wasio na akili,
“Wote ambao ni wajinga na waje hapa!

5 eNjooni, mle chakula changu
na mnywe divai niliyoichanganya.

6 fAcheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi;
tembeeni katika njia ya ufahamu.

Copyright information for SwhKC